Scroll To Top

end time knowledge, Prophecy for today end time knowledge, Prophecy for today
Isaya 11:6-9
6 “Mbwa-mwitu naye atakaa pamoja na mwana-kondoo, chui atalala pamoja na mwana-mbuzi, ndama na mwana-simba na kinono pamoja; Na mtoto mdogo atawaongoza.
7 Ng’ombe na dubu watalisha; Watoto wao watalala pamoja; Na simba atakula majani kama ng'ombe.
8 Mtoto anyonyaye atacheza penye tundu la nyoka, na mtoto aliyeachishwa atatia mkono wake katika tundu la nyoka.
9 Hawatadhuru wala hawataharibu katika mlima wangu wote mtakatifu; kwa maana dunia itajawa na kumjua Bwana, kama vile maji yaifunikavyo bahari.
end time knowledge, Prophecy for today

Siku Uumbaji Unavyoona Kisasi

Na Jacquelyn Fedor

Ilitafsiriwa Na David Odhiambo
2026-03-23


Tafadhali bofya maandishi ya samawati hafifu kwa maelezo zaidi


Kama tulivyokuwa tukijifunza katika mafundisho machache iliyopita, kila kitu chenye pumzi, mimea, wanyama, vitu vilivyo mbinguni na pia vyote vilivyo duniani ni sehemu ya Yeshua na vimeumbwa kutoka kwa sehemu yake. Kwa hivyo Yeye ndiye kiini cha vitu vyote, au kinachoshikilia vitu vyote pamoja, kwa hivyo bila Yeye hatuwezi kuwepo.
Uelewa wa taarifa hii hutoa mwanga mpya kuhusu maisha ya Ufalme. Uumbaji wote uliumbwa awali ili kuingiliana, kuleta uhai kwa kila mmoja, lakini kupitia kutotii kwa Adamu na Hawa badala yake tumekuwa hasara kwetu sisi wenyewe, dunia, na viumbe vyote vilivyomo! Walipovutwa kutoka Paradiso hadi katika ulimwengu huu wa udanganyifu ulioundwa na Shetani, ni wazi hawakuwa sawa tena, na kila kitu walichokuwa nacho kilitoka nje ya usawa pia. Kumbuka, dunia yenyewe ilipewa mwanadamu, pamoja na kila kitu kilichomo, kwa hivyo ni wazi jinsi uumbaji ungekuwa na mambo na wanadamu.
Kwa bahati nzuri Yeshua alitengeneza njia ya kila kitu kurejeshwa, lakini yote haya yanategemea ubinadamu kufananishwa tena katika mfano wa Yeshua ili wao na wote walio kuwa na utawala juu yao wawe katika usawa au kwa mdundo mkamilifu na ulimwengu wote kama ilivyokuwa mwanzo. Kwa mara nyingine tena, maisha katika sayari ya dunia yatarudishwa kwenye hatima iliyoamuliwa na Baba. Unaona, viumbe vyote vinateseka chini ya utawala mkuu wa Shetani na wao pia wanataka kuona Ufalme ukisimamishwa tena na mapenzi kamili ya Mungu yakitendeka kuhusu viumbe vyote vilivyo hai. Kwa kweli, utaona tunapoangalia nyuma katika historia, kwamba katika nyakati tofauti wakati mwanadamu alipojaribu kujiondoa kutoka kwa utawala mwovu wa Shetani, uumbaji uliwasaidia.
Kwa upande mwingine, wanadamu walikuwa waovu sana katika siku za Nuhu kiasi kwamba Bwana alichoka kuwavumilia, alijuta hata aliwaumba, hata akajuta kwamba aliwaumba wakazi wengine wa dunia kwa sababu asili ya Shetani ilikuwa imewapa wao pia. Kwa amri ya Mungu maji ya gharika yaliwameza. Tazama Sodoma na Gomora. Haikuwa bunduki na vifaru vilivyochukua miji hiyo, haikuwa hata silaha za siku hiyo, ilikuwa moto na kiberiti vilivyotumwa kutoka mbinguni ili kuangamiza. Na katika siku ya Musa, haikuwa meli ya kivita iliyowachukua Israeli wa zamani kuvuka bahari kutoka kwa Farao, bahari zenyewe zilirundikana na kuwaruhusu kutembea kuvuka viatu vikavu au kwenye nchi kavu.
Kutoka 15:8-10
8 Na kwa pumzi ya pua zako maji yalikusanyika pamoja; mafuriko yalisimama wima kama rundo; vilindi viliganda katikati ya bahari.
9 Adui akasema, ‘Nitawafuatia, nitawapata, nitagawanya nyara; hamu yangu itashibishwa nao. Nitatoa upanga wangu, mkono wangu utawaangamiza.’
10 Ulivuma kwa upepo wako, bahari ikawafunika; walizama kama risasi katika maji yenye nguvu.
Hebu tusome kutoka Isaya 30:23-26
23 Ndipo Yeye (Bwana) atatoa mvua kwa mbegu zako ulizopanda ardhini, na mkate wa mazao ya ardhi; itakuwa nono na tele. Katika siku hiyo ng'ombe wako watakula katika malisho mapana.
24 Kadhalika ng'ombe na punda wachanga wanaolima ardhi watakula chakula kilichopozwa, kilichopepetwa kwa koleo na pepeo.
25 Kutakuwa na vijito na mito ya maji juu ya kila kilima na mlima mrefu, siku ya machinjo makubwa, minara itakapoanguka.
26 Zaidi ya hayo, nuru ya mwezi itakuwa kama nuru ya jua, na nuru ya jua itakuwa mara saba, kama nuru ya siku saba, siku ambayo Bwana atafunga jeraha la watu wake na kuponya pigo la jeraha lao.
Bwana alitumia uumbaji kupigania Israeli ya zamani na pia kuibariki. Kwa nini tunafikiri itakuwa tofauti katika siku ya Bwana leo? Kwa kweli, tukiangalia Luka 21:25-26, tutaona kwamba kwa kweli uumbaji utatumika mwishoni.
Luka 21:25-26
25 “Na kutakuwa na ishara katika jua, mwezi, na nyota; na duniani dhiki ya mataifa, wakishangaa, bahari na mawimbi yakivuma;
26 mioyo ya watu ikizimia kwa hofu na kutazamia mambo hayo yatakayo upata ulimwengu, kwa maana nguvu za mbinguni zitatikisika.
Kumbuka katika Ufunuo 16 kwamba ilisema kutakuwa na tetemeko la ardhi, ambalo halijapata kuonekana hapo awali.
Ufunuo 16:17-18
17 Kisha malaika wa saba akamwaga bakuli lake hewani, na sauti kubwa ikatoka katika hekalu la mbinguni, kutoka katika kiti cha enzi, ikisema, “Imekwisha!”
18 Na kulikuwa na kelele na radi na ngurumo; na kulikuwa natetemeko kubwa la ardhi, tetemeko kubwa na ambalo halijawahi kutokea tangu wanadamu kuwapo duniani.
Je, hii inaweza kuwa ni kiasi gani cha ulimwengu wa Shetani na watu wake wanateketezwa kama katika siku ya Kora, wakati dunia ilipofunguka na kumeza familia yake, mifugo yake na yote yanayomhusu? Kumbuka ngurumo, radi, na Neno linazungumzia mawe makubwa ya mvua ya mawe mwishoni, kwamba bahari zitanguruma!
Je, unaweza kufikiria uumbaji unapogeuka uovu, hii itakuwaje!! Inasema mwanadamu atakimbilia milimani na kulia miamba ianguke juu yake! Kwa kweli, katika historia yote tunaona mahali ambapo Mungu ameruhusu uumbaji kulipiza kisasi ili tujue ni ukweli! Inatisha unapoifikiria! Fikiria juu yake, vimbunga, kimbunga, mvua kubwa, mvua ya mawe, maporomoko ya matope, tsunami, moto mkali, matetemeko ya ardhi, yote yanaenda kwa wakati mmoja huku uumbaji ukipiza kisasi.
Hebu tuangalie Isaya 24:4-6
4 Dunia inaomboleza na kufifia, dunia (ardhi) inadhoofika na kufifia; watu wenye kiburi wa dunia wanadhoofika (wanakuwa dhaifu).
5 Dunia pia imetiwa unajisi chini ya wakazi wake, (hii ndiyo sababu) kwa sababu wamevunja sheria, wamebadilisha amri, wamevunja agano la milele.
6 Kwa hiyo laana imeila dunia, na wale wanaokaa ndani yake wanaukiwa. Kwa hiyo wakazi wa dunia wanateketea, na watu wachache wamebaki. (Uumbajiunashinda!)
Je, huo si unabii kuhusu siku za mwisho!!
Hebu tuangalie Waamuzi 5:20-21 sasa na tutaona kwamba hata mbingu, pamoja na dunia, zilipigana kwa ajili ya Debora na Baraka.
20 Walipigana kutoka mbinguni; nyota kutoka kwenye njia zao zilipigana na Sisera.
21 Mkondo (mto) wa Kishoni uliwasomba, mto ule wa kale, mto wa Kishoni. Ee nafsi yangu, songa mbele kwa nguvu!
Mahali pengine ambapo mwanadamu na uumbaji walifanya kazi pamoja panaonekana katika Yoshua 10.
Yoshua 10:12-13
12 Ndipo Yoshua akasema na Bwana siku ile Bwana alipowatoa Waamori mbele ya wana wa Israeli, naye (Yoshua) akasema mbele ya Israeli: “Jua, simama wima juu ya Gibeoni; na Mwezi, katika Bonde la Aiyaloni.”
13 Basi jua likasimama wima, na mwezi ukasimama, hadi watu walipolipiza kisasi juu ya adui zao. Je, haya hayakuandikwa katika Kitabu cha Yashari? Basi jua likasimama wima katikati ya mbingu, wala halikuharakisha kuchwa kwa kama siku nzima.
Unaona kila kitu ambacho ni sehemu ya Yeshua siku moja vitakusanywa dhidi ya adui kama kitu kimoja, kwa ujumla. Itakuwa vita kati ya uumbaji unaolingana na Mungu ili kuharibu kila kitu kwenye sayari hii ambacho si chake na kisichofanya kazi na ujumla. Mwanadamu ataomba, atasifu, atacheza ili kukanyaga kichwa cha adui ili kumrudisha adui duniani. Mbingu zitatuma radi yao, ngurumo zao, na mvua ya mawe yao. Pepo nne za dunia zitafunguliwa, bahari zitanguruma na dunia itafungua kinywa chake kumeza kila kitu kibaya kilicho karibu nayo (tetemeko kubwa la ardhi kwenye bakuli la saba). Spishi tofauti za wanyama ambao wametendewa vibaya kwa ajili ya mchezo wa mwanadamu wataruhusiwa kulipiza kisasi kwa wale waliowatendea vibaya. Ukatili, ukosefu wa heshima kwa maisha ya uumbaji wa Mungu ambao kwa kweli ulikuwa sehemu ya Mwanawe wataona ghadhabu ya Mungu na kupata hisia zake kuihusu.
Kwa bahati nzuri, kwa wale wanaopenda uumbaji, watiifu wanaotaka kurudi katika umoja na Bwana wao, kuna mahali pa usalama, makazi na amani. Ni Maskani ya Daudi, iliyo na watoto wa Mungu waliodhihirishwa.
Hosea 2:18-23 ilizungumzia wakati huu.
18 Katika siku hiyo mimi (Bwana) nitafanya agano kwa ajili yao na wanyama wakondeni (hawatadhuriwa na wanyama), na ndege wa angani, na vitu vitambaavyo vya ardhini. Nitavunja upinde na upanga wa vita kutoka duniani, ili niwalaze salama.
Sasa tazama ahadi nzuri kwa watiifu!!
19 “Mimi (Bwana) nitakuposa uwe wangu milele; naam, nitakuposa kwa haki na uadilifu, na kwa fadhili na rehema;
20 Nitakuposa uwe wangu kwa uaminifu, nawe utamjua Bwana.
21 “Itakuwa siku hiyo nitajibu,” asema Bwana; “Nitajibu mbingu, nazo zitaijibu dunia.
22 Dunia itajibu kwa nafaka, kwa divai mpya, na kwa mafuta; nazo zitaijibu Yezreeli.
23 Ndipo nitakampanda nchi kwa ajili yangu mwenyewe, nami nitamhurumia yeye ambaye hakupata rehema; ndipo nitakapowaambia wale ambao hawakuwa watu wangu, ‘Nyinyi ni watu wangu!’ Nao watasema, ‘Wewe ni Mungu wangu!’ "
Labda kwa taarifa hii mwanadamu anaweza kuanza kutazama mambo kutoka mtazamo tofauti, hasa akikumbuka kwamba vitu vyote ni sehemu ya Yesu Kristo. Wanapotafakari jinsi vitu vyote vinavyoingiliana, jinsi ambavyo ni sehemu ya ustawi wa kila kimoja, jinsi vinavyoshiriki katika kusaidiana, na wanapokumbuka kwamba magonjwa, maumivu na kifo havikuwa sehemu ya uumbaji wa Mungu, hadi kutotii kwa mwanadamu, labda watabadilisha mtazamo wao na watabadilisha jinsi wanavyofikiria kuhusu uumbaji.
Kwa mfano, kama ilivyofundishwa hapo awali, lishe ya Mwanzo ilihusisha mimea yote, na katika Isaya 11 tunaona kwamba ufalme wa wanyama uliorejeshwa ulirudishwa kwenye lishe hiyo. Katika Ufalme wa Mungu hakutakuwa na wala nyama. Nimrod, mwanzilishi wa Babeli, alikuwa na asili ya baba yake Shetani. Alikuwa mwindaji hodari na hakujali sana maisha. Hapo awali tuliumbwa kwa mfano wa Mungu wa upendo na bado ubinadamu mwingi, kama Nimrod, umechukua asili ya baba yao, Shetani. Alitaka kuwa mkuu zaidi, nambari moja, bora zaidi, aliyekuja kuua, kuiba na kuharibu! Ili kuwa wala nyama kitu lazima kiuawe.
Nataka Kupatikana miongoni mwa wale wanaomwimbia Mungu sifa mwishowe, sambamba na ulimwengu wote. Kila kiumbe hai kina wimbo unaouona, na sitaki kuwa mtu anayeharibu uumbaji wa Mungu na kwa hivyo milele anazuia wimbo wao kumfikia, kutoka kwa kumwimbia sifa. Anaona, anajua, Neno linasema Anaona kila shomoro mdogo anapoanguka. Anajua kila nywele kichwani mwetu, Anaona yote, anajua yote, na simulizi limerekodiwa ambalo litashughulikiwa Siku ya Hukumu!
Unaona, Mungu aliumba ulimwengu kupitia fomula zilizohesabiwa kikamilifu na kile Alichokiumba kwa ajili ya sayari hii kilikusudiwa kuishi kwa utulivu wa amani katika dunia nzuri. Kama tungekuwa watiifu, sehemu kubwa ya dunia ingekuwa imeigwa kufikia sasa, na kupanuliwa kutoka bustanini hadi makao mazuri, yenye rutuba kwa wanadamu wote na uumbaji wote kama ilivyopangwa awali na Mungu.
Badala yake, angalia tulichonacho, angalia tulichokifanya kwa sayari yetu! Sijui tuna muda gani zaidi, lakini tunapozingatia mambo haya, labda tunaweza kutubu, kugeuka kutoka kwa njia zetu mbaya na kuwa wale wanaopata nafasi yetu katika Yeshua, kwa usawa na sehemu ya yote.
2 Petro 3:10-12
10 Lakini siku ya Bwana itakuja kama mwizi usiku, ambayo mbingu zitatoweka kwa mshindo mkuu, na viumbe vya asili vitayeyuka kwa moto mkali; dunia na kazi zilizomo ndani yake zitateketea.
11 Basi, kwa kuwa vitu hivi vyote vitayeyuka, imewapasa nyinyi kuwa watu wa namna gani katika mwenendo mtakatifu na utauwa (je, tutapatikana watakatifu na tukitazamia mwisho),
12 tukitazamia na kuharakisha kuja kwa siku ya Mungu, ambayo kwa hiyo mbingu zitayeyuka, zikiwa zinawaka moto, na viumbe vya asili vitayeyuka kwa moto mkali?
Hili ndilo kundi ambalo ningependa kuwa sehemu yake, lile linalopatikana katika Waefeso 1:10.
10 ili katika wakati mkamilifu wa nyakati apate kukusanya pamoja vitu vyote katika Kristo, vilivyo mbinguni na vilivyo duniani—ndani yake.
Unaona, ambapo Yeshua amekusanya vitu vyote pamoja ndani yake, kuna usalama, malazi na amani. Yeye ndiye Nchi ya Ahadi ambayo Mungu alisema tunaweza kuingia na Ufalme wa Mungu utaanzishwa. Wale wanaotii njia za Yeshua na kuweka mavazi yao safi, Neno lilisema, pia watapewa haki ya kula kutoka kwa Mti wa Uzima.
Ufunuo 22:14
14 Heri wale wazishikao amri zake, wapate haki ya kuuendea mti wa uzima, na kuingia mjini kwa malango.
Ufunuo 21 utakuwa ukweli wakati huu ambao hakika nataka kuwa sehemu yake. Vipi kuhusu wewe?
Ufunuo 21:1-5
1 Sasa nikaona mbingu mpya na dunia mpya, kwa maana mbingu ya kwanza na nchi ya kwanza (ulimwengu wa Shetani) zilikuwa zimepita. Pia hapakuwa na bahari tena (bahari ya wanadamu walioanguka).
2 Kisha mimi, Yohana, nikaona mji mtakatifu, Yerusalemu Mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, ukiwa tayari kama bibi arusi aliyepambwa kwa mumewe.
3 Nikasikia sauti kubwa kutoka mbinguni ikisema, Tazama, maskani ya Mungu iko pamoja na wanadamu (hema ya Daudi), naye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, naye atakuwa Mungu wao.
Sawa, sikiliza ahadi zetu!! 4 Na Mungu atafuta kila chozi kutoka machoni mwao; hakutakuwa na kifo tena, wala maombolezo, wala kilio. Hakutakuwa na maumivu tena, kwa maana mambo ya kwanza yamepita.” (hatimaye, hisia ya ustawi!!)
5 Kisha yeye aliyeketi kwenye kiti cha enzi akasema, “Tazama, nayafanya yote kuwa mapya.” Akaniambia, “Andika, kwa maana maneno haya ni kweli na ya uaminifu.”
Kwa kumalizia, hebu tumsifu Yeshua kwa kufanya haya yote yawezekane na ahadi yenye uhalisia kamili kwa wale wanaopenda uumbaji na ni watiifu!! Siku ije haraka na viumbe vyote vione kisasi!
Bofya vichwa ili kucheza nyimbo zinazohusiana na mada hii
Hasten The Day
Give Glory To The Lamb
Safety, Shelter And Peace

Tumia (+) kupanua uorodheshaji ndani ya kikundi.

2015 + -
2012 + -
2011 + -

Submit Your Site To The Web's Top 50 Search Engines for Free!