Scroll To Top

end time knowledge, Prophecy for today end time knowledge, Prophecy for today
Isaya 11:6-9
6 “Mbwa-mwitu naye atakaa pamoja na mwana-kondoo, chui atalala pamoja na mwana-mbuzi, ndama na mwana-simba na kinono pamoja; Na mtoto mdogo atawaongoza.
7 Ng’ombe na dubu watalisha; Watoto wao watalala pamoja; Na simba atakula majani kama ng'ombe.
8 Mtoto anyonyaye atacheza penye tundu la nyoka, na mtoto aliyeachishwa atatia mkono wake katika tundu la nyoka.
9 Hawatadhuru wala hawataharibu katika mlima wangu wote mtakatifu; kwa maana dunia itajawa na kumjua Bwana, kama vile maji yaifunikavyo bahari.
end time knowledge, Prophecy for today

Tunakaribia

Na Jacquelyn Fedor

Ilitafsiriwa Na David Odhiambo
2025-06-02


Hapo mwanzo Mungu alisema “iwe nuru” na kukawa na nuru. Alikuwa akizungumza na nani?
Wakolosai 1:15-16 inatuambia,
15 Yeye ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote.
16 Kwa kuwa katika yeye (Yesu) vitu vyote viliumbwa vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana, ikiwa ni viti vya enzi au watawala au wakuu au wenye mamlaka. Vitu vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake.
Katika Mwanzo 1:26 Mungu akasema, na tumfanye mtu kwa sura yetu au kwa mfano wetu. Hakuwa akizungumza na malaika kama baadhi ya makanisa ya ulimwengu yanavyofundisha, alikuwa akizungumza na Mwanawe ambaye alileta vitu vyote.
Mwanzo 1:26
26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi. (Unaona sisi ni akina nani tunaporejeshwa?)
Sasa, unaposoma Zaburi 8:4-5 inasema tuliumbwa chini kidogo kuliko malaika?
Zaburi 8:4-5
4 Mtu ni nini, ee Mungu, hata umfikirie, wanadamu ni nani hata umjali?
5 Kwa maana umemfanya mdogo punde kuliko malaika, na umemvikataji ya utukufu na heshima.
Ikiwa tuliumbwa kwa mfano wa Mungu na Mwanawe, mtu amechanganyikiwa kweli! Mungu si malaika! Ukitazama neno malaika jinsi linavyofasiriwa katika andiko hilo katika Strongs Concordance hata hivyo, utaona maana yake elohim, sasa hii inaleta maana zaidi na inapatana na Zaburi 82:6.
Zaburi 82:6
6 Mimi nimesema kuwa, “Ninyi ni miungu, na ninyi nyote ni wana wa Aliye juu (si malaika)
2 Wakorintho 3:18
18 Lakini sisi sote, ambao nyuso zetu hazikufunikwa (pazia la udanganyifu lililoondolewa), tunaona kama kioo utukufu wa Bwana (si malaika), tunabadilishwa tufanane na mfano huo kutoka utukufu hadi utukufu, kupitia Roho ya Bwana,
Sasa tunajua bora, hatuko jinni ya Malaika, naa fundisho linguine la uwongo limefunuliwa na ukweli!
Ukweli wa mambo ni kuwa, jambo hili lilifichwa kwa sababu zisizo eleweka, kwasababu barua ya blue latter ilikubali kuwa halitasfiriwi kama Malaika katika tafsiri ya kitambo. Ilitasfiriwa kwa usahihi kama Elohim katika Biblia ya awali ya Kiebrania. Tazama maoni hapa chini.
Somo la Bibilia ya blue letter “Zaburi 8:5 kiebrania Elohim, Mungu; Mila ya kiyahudi, septuagit, syriac, targum hutafsiri kama Malaika.”
Kwa maneno mengine, Zaburi 8:5, katika Biblia ya awali ya Kiebrania hapo awali ilikuwa Elohim, Mungu. Kwa sababu ya mila ya Kiyahudi, maandiko yalipotafsiriwa kutoka kwa Kiebrania hadi Kigiriki na Kiarabu, Septuagint, Syriac na Targumi, yalibadilishwa na kutafsiriwa kama malaika.
Je, haya yote yana tofauti gani?
Ili kuelewa sisi ni nini au nani, lazima tuchague maarifa ya shetani kutoka kwa ukweli au hatutakuwa kamwe kwa sura yake au maumbile yake kurithi ahadi zilizotolewa kwa Watoto wa mungu. Kumbuka alichosema katika Wagalatia 3.
Wagalatia 3:27-29
27 Maana nyinyi nyote mliobatizwa katika Kristo mmemvaa Kristo.
28 Hakuna Myahudi wala Mgiriki, mtumwa wala huru, hakuna mwanamume wala mwanamke; kwa maana nyinyi nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu.
29 Na kama nyinyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa uzao wa Abrahamu, na warithi sawasawa na ahadi.
Wagalatia 4:1 inafunua kwa nini huenda hatujapokea urithi wetu bado.
1 Sasa nasema kwamba mrithi, akiwa bado mtoto, hana tofauti kabisa na mtumwa, ingawa mali yote ni yake.
Na, ikiwa sisi ni wapuuzi, Shetani ataendelea kuleta kushindwa katika maisha yetu. Unaona, sisi sio tu elohim, sisi sio watoto kwa maana iliyotumiwa hapo juu pia! Ukitafuta neno mtoto jinsi lilivyotumika katika andiko hilo katika kamusi ya Strongs utaona maana yake, mtoto mchanga, asiyena uwezo wa kuongea. Sisi tunaongea mengi! Tunaweka ukweli nje kwa haraka kama vile Bwana anavyotuonyesha na wale wanaoisoma na kuijadili na wengine wanaisema kwa upepo kulingana na Ezekieli 37:9.
Ezekieli 37:9
9 Tena akaniambia, “Itabirie pumzi, tabiri mwanadamu, na kuiambia pumzi, Bwana MUNGU asema hivi, “Njoo kutoka katika pepo nne, Ee pumzi, na kuwapulizia hawa waliouawa (waliokufa katika dhambi na ujinga), ili wapate kuishi”.
Tunapozungumza na marafiki na familia pumzi yetu ni kutuma ukweli kwa upepo! Tunapohubiri, kufundisha, kusifu na kuomba ukweli unaenda nje kwa upepo. Sisi ni elohim, wana wa Mungu tunenao kweli ya Mungu! Tuko njiani kuelekea kuwa katika sura ya Kristo! Tukiwa na maarifa na hekima ya Mungu katika akili zetu na kuongezwa kwenye hifadhidata yetu na sheria ya Baba iliyoandikwa kwenye mioyo na akili zetu pia, mitazamo, tabia na mawazo yetu hubadilika na tunaanza kuzaa matunda yaliyoorodheshwa katika Wagalatia 5:22-23 katika maisha yetu ya kila siku.
Wagalatia 5:22-23
22 Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu, wema, fadhili, uaminifu,
23 upole, kujizuia. Kinyume na hivyo hakuna sheria.
Sasa tunafanya maendeleo ya kweli kuelekea kuwa watoto wa Mungu waliodhihirishwa, aina tofauti, spishi yake mpya!
Zaburi 102:18 ilitabiri jambo hili kuwa.
18 Haya yataandikwa kwa ajili ya kizazi kijacho, kwamba watu ambao bado hawajaumbwa (si jamii ya Adamu, viumbe vipya) wapate kumsifu Yehova.
Kama vile dunia ilivyoimbwa kuwa, ndivyo dunia mpya itarudishwa pia kwa wimbo wa spishi mpya.
Kupitia kizazi hiki kipya uwongo na mafundisho ya uongo yanayofundishwa kwa mwanadamu yatafichuliwa pia! Roho Mtakatifu alipofichua ukweli kuhusu nyoka wa shaba kwa mfano, hatua kubwa kuelekea urejesho wetu ilifanywa. Ikawa rahisi zaidi kuzaa tunda la Roho katika roho zetu, na asili yetu kwa hiyo ilianza kubadilika sana. Tunapoanza pia kuelewa maarifa ambayo Hawa alichagua ni nini miundombinu ya ulimwengu huu inaundwa, tunapoteza imani na ulimwengu, mifumo yake na kwa hakika elimu yake ya juu! Tunaanza kuelewa uwongo wa hata kujaribu kutatua shida za ulimwengu. Kwanza, ulimwengu huu ni wa Shetani na si sehemu ya Ufalme wa Mungu hata kidogo. Kwa hiyo imekusudiwa kuharibiwa wakati Ufalme wa Mungu utakapodhihirishwa duniani hata hivyo! Sio maana sana katika kujenga mtindo mzuri wa maisha ikiwa huu ndio mpango ulioamriwa wa Mungu wetu mkuu uko pale! Kwa hivyo ikiwa upako wa Shetani na ushawishi mbaya unafunika na kuchafua kila kitu na kila mtu katika ulimwengu, hakuna maana kubwa ya kuwakasirikia watu kwa matendo yao mabaya pia? Wao ni vikaragosi tu na bila hatia hata hawajui, kwa hivyo hisia zetu kwao zinaanza kubadilika pia. Hasira yetu inaelekezwa kwa kiumbe sahihi, sababu ya kweli ya matatizo yetu yote, Shetani!
Wakati ulimwengu unaendelea kupigana, kujaribu kutatua shida zao wenyewe, tumejifunza kupumzika kwa Mungu! Sasa tunabadilika kweli! Tunaacha kujitahidi, kusukuma, kujaribu kufanya mambo kutokea kwa sisi binafsi na kuanza kuona picha kubwa zaidi, urejesho wa viumbe vyote! Tunapoendelea kunyonya ujuzi Wake na kusaga tunda la hekima yake, akili zetu hupona kutokana na shambulio la Shetani dhidi ya Hawa. Uwongo na mafundisho ya uwongo yaliyofundishwa kwa wazao wa Adamu ambayo yamesababisha mtazamo uliopotoka wa mwanadamu juu ya maisha kwa ujumla yatafichuliwa na mahali pake pawe na ukweli. Akili huanza kupona, hali ya moyo inabadilika na tunaanza kurejeshwa! Je, unaelewa, mabadiliko haya ya akili na moyo lazima yatendeke kabla ya miili yetu mingine kurejeshwa? Katika bustani Adamu na Hawa walitoa mioyo na akili zao kwa Shetani na kukubali maarifa ya Shetani au Lusifa. Kwa hivyo tena, hii lazima iwe ya kwanza kubadilishwa! Mungu amefanya iwe wazi na rahisi kadiri iwezekanavyo kwetu kuchagua lililo sawa na lisilo sahihi na kufanya mabadiliko. Aliandika sheria zake kwenye mioyo na akili zetu ili sote tupate nafasi ya kushika amri zake ili tuweze kuthibitisha upendo wetu kwake.
Waebrania 8:10
10 Kwa maana hili ndilo agano nitakalofanya na nyumba ya Israeli baada ya siku hizo (siku ya 7), asema Bwana: Nitaweka sheria zangu katika nia zao, na katika mioyo yao nitaziandika; nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.
Yohana 14:21
21 Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye. Naye anipendaye atapendwa na Baba yangu, nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.”
Elewa, kutotii kwa jozi ya kwanza ilikuwa mwanzo wa uovu wote duniani! Hawa alipofungua nia yake kwa Mawazo ya shetani na ufahamu wake, moyo wake ukawa na wivu juu ya ufahamu wake Dhahiri na hekima. Kutaka kufahamika au “lazima niwe nambari moja” ilimshawishi, kisha likashirikiana na moyo na nia yake na yeye akalegea. Kwa majibu haya kwa shetani kifo na kuoza sio tuk wake na Adamu bali kwa wote waliotawala. Kumbuka Mwanzo 1:26.
Hapa sasa kuna sehemu ya maandiko ambayo inatuonyesha zaidi kile ambacho lazima kitokee kabla ya urejesho wa uumbaji hata hivyo Isaya 11 inafunua urejesho wa uumbaji mstari wa 6,7 na 8 inaonyesha uumbaji wote tayari umerejeshwa na kile kinachoileta katika udhihirisho kinafafanuliwa katika mstari wa 9. Wacha tuangalie urejesho wa uumbaji kwanza.
Isaya 11:6-8
6 Mbwamwitu ataishi pamoja na mwanakondoo, chui watapumzika pamoja na mwanambuzi, ndama na mwanasimba watacheza pamoja; na mtoto mdogo atawaongoza.
7 Ng’ombe na dubu watakula pamoja; ndama wao watapumzika pamoja; na simba atakula majani kama ng'ombe.
8 Mtoto mchanga atacheza penye tundu la nyoka, na mtoto atatia mkono wake katika tundu la nyoka wa sumu.
Sasa hapa kuna ufunguo wa kile kinacholeta haya yote kuwa!
Isaya 11:9
9 Hawatadhuru wala kuharibu katika mlima wangu wote mtakatifu (hakuna kuua, wala vita, wala kuua wanyama wa kula, wala kukata vichwa vyao kwa ajili ya mapambo juu ya ukuta), kwa maana dunia itajawa na maarifa ya Bwana (mana safi, ufahamu wa siku ya nane, maarifa ambayo Danieli aliambiwa ayafunge mpaka wakati wa mwisho, yaliyomo ndani ya mihuri ya Ufunuo). Kama maji ya Bahari.
Kuona maandiko haya mazuri kuwa ukweli kuna mambo ambayo lazima tutimize kama mwili wa Kristo na malengo ambayo lazima tufikie kama mtu binafsi. Kwanza kabisa, nyumba ya Daudi lazima isimamishwe, ionekane na kutambuliwa ili Bwana aweze kutoa mwongozo kwa ajili ya kujengwa upya kwa Ufalme Wake kwa wale wanaokuja kwenye mlima wa Mungu. Mawe yaliyo hai ambayo ameijenga maskani hii ni ofisi zake, serikali yake, wale anaowaongoza watu wake kuwapitia. Kutoka katika nyumba hii atawasaidia watu wenye nia ya Ufalme kurejeshwa kwa sura ya Kristo, kwa mara nyingine tena kuwa katika sura ya Mungu, na kupatana na mapenzi yake kama hapo mwanzo. Isaya alitabiri jambo hili zamani sana ili tuweze kulitambua.
Isaya 2:2-4
2 Basi itakuwa katika siku za mwisho, mlima wa nyumba ya Bwana (serikali yake) utawekwa imara juu ya milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na mataifa yote yatamiminika humo.
3 Watu wengi watakuja na kusema, “Njoni, twende juu mlimani kwa Bwana, nyumbani kwa Mungu wa Yakobo, naye atatufundisha njia zake, nasi tutakwenda katika mwongozo wake”. Kwa maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la Bwana kutoka Yerusalemu.
4 Yeye atasuluhisha mizozo ya mataifa, na kuwakemea watu wengi; watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu; taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena.
Matokeo ya mwisho ya mafunzo haya ya watu wa Mungu ni kurejeshwa kwa viumbe vyote kama inavyoonekana katika Warumi.
Warumi 8:21
21 kwa sababu viumbe vyenyewe navyo vitakombolewa kutoka katika utumwa wa uharibifu (au kifo) na kuingia katika uhuru wa utukufu (uhuru kutoka kwa Shetani na ulimwengu wake) wa watoto wa Mungu.
Hebu tubadili mwelekeo sasa na tujadili kwa nini kuna haja ya mabadiliko mengi. Kama tunavyojua kutoka kwa somo lililopita, Shetani alikuwa kerubi, mfano wa malaika aliyeumbwa na Bwana. mkamilifu kwa kila njia, mwenye karama na upako na aliyeteuliwa kuifunika dunia nzima na uumbaji wote wa Mungu juu yake. Alikuwa na ala za muziki zilizoumbwa ndani yake hapo mwanzo ili kutufundisha jinsi ya kumsifu Bwana. Kwa mwongozo wake tulipaswa kuishi maisha ya ajabu katika mapenzi makamilifu ya Mungu. Alitiwa mafuta kuwa mlinzi aliyevaa chuma dhidi ya jambo lolote ambalo lilitishia ustawi wetu. Badala yake aliamua kutawala dunia, kweli alipenda uzuri wake na uwezo wake na kiburi chake kilimshawishi kuwa na uwezo wa kushindana na Mungu kwa viwango vyote na akampa mashindano kuwa mkuu! Kwa sababu ya uovu wake kiumbe huyu aliyeumbwa kikamilifu akawa mwovu kabisa na kwa hiyo akachafua kabisa kila kitu alichokuwa kulinda na kufunika, akiwemo ubinadamu!
Je, unaweza kuona jinsi yote yangepotea kama isingekuwa dhabihu ya Yeshua na mpango ulioamriwa wa Baba wa ukamilifu na urejesho wetu? Kwa kuwa Baba aliumba vitu vyote kupitia Yeshua, Anajua kabisa jinsi ya kurejesha vitu vyote pia! Je, unakumbuka Wakolosai 1:16?
Wakolosai 1:16
16 Maana katika yeye (Yeshua) vitu vyote viliumbwa vilivyo mbinguni na vilivyo duniani, vinavyoonekana na visivyoonekana, ikiwa ni viti vya enzi au watawala au wakuu au mamlaka. Vitu vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake.
Nilirudia andiko hili ili uweze kuona jinsi Luka 12:7 inavyoweza kuwa uhalisi. Anamjua kwa undani kila mmoja wetu, alituumba, kwa hivyo ukamilifu wetu wa asili umehakikishwa.
Luka 12:7
7 Lakini hata nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote. Basi, msiogope; ninyi ni wa thamani kuliko shomoro wengi.
Kwa hivyo tunaweza kufanya nini kibinafsi ili kudhihirika kama mwana wa Mungu? Kwanza kabisa, soma neno, karamu juu ya wakati wa mwisho wa siku ya nane ufahamu wa maandiko. Hii itawezesha mawazo na njia zetu kusawazisha Mawazo na mpango wa asili wa Mungu kwa dunia na uumbaji Wake wa awali ulioundwa kikamilifu. Wote lazima wawe katika maelewano mwishowe ili wawe sehemu ya ulimwengu kama Baba alivyokusudia. Kumbuka sisi sote ni sehemu ya jumla.
Waefeso 1:10
10 ili katika kipindi cha utimilifu wa nyakati, (pasopokuwa na sheria yeyote) avikusanye pamoja viumbe vyote kila kitu mbinguni na duniani, chini ya kristo.
Mwanzoni mwa mafundisho huu tulijadili jinsi sisi, watu wa siku ya nane tulivyo elohim na si watoto tena. Sisi ni watu ambao tunataka kuona uumbaji wote ukirejeshwa lakini kumbuka, ili kuona hili likitimizwa ni lazima kwanza tujidhihirishe kama watoto wa Mungu, tuwe tena katika sura yake na kwa mfano wake. Je, hii hutokeaje? Tunakuwa mwili wa mwili wake tunaposhiriki mkate wa ushirika. Sasa, kwa kuwa tumekula mwili wake, kama kweli rhemas kwetu sisi kujazwa na mwanga na kufanana zaidi na zaidi kama Neno.
Yohana 1:1,4
1 Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
4 Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu.
Kwa kuwa maisha Yake yako katika damu Yake, tunapokunywa divai ya ushirika DNA Yake inakuwa yetu na jinsi maisha yetu yalivyo katika damu yetu pia, kwa hiyo tunakuwa mmoja Naye! Kwa hivyo sasa tumekuwa mwili wa mwili wa Neno na tuna chembechembe zake, DNA Yake, lakini bado hakuna mfumo wa kiunzi, hakuna dutu, hakuna mfupa! Hatuwezi kuwa mwili bila mifupa! Kwa hivyo nilitazama mfupa kwenye Strongs Concordance na ilielezea mengi! Alinijibu maswali mengi ambayo sijaelewa. Nambari ya kwanza, neno mfupa kama nomino ni ya kike (Bibi arusi)! Kama kiwakilishi (kundi la maneno yanayoelezea au kumaanisha kitu sawa na nomino) sikiliza hii, mwili uleule! Mmoja pamoja Naye! Inapendeza zaidi! Neno mfupa linatokana na mzizi wa awali wenye maana ya kufunga haraka, kufunga macho. Kumbuka Adamu na Hawa walipoanguka macho yao yakafumbuka na wao kutoka wakati huo, kwa sehemu kubwa waliona hali hili ya kawaida pekee. Naam mfupa huenda kufunga macho, funga! Je, sisi pia tutaweza kuona falme zote mbili kama walivyofanya jozi ya kwanza kabla hawajaanguka? Inakuwa bora zaidi! Inamaanisha kufanya nguvu, kuwa mkuu, hodari. Katika Danieli 12:7 tunaambiwa nguvu za watu watakatifu zimevunjwa au kuvunjwa. Tunapokutana pamoja kama Mwili Wake au kama Bibi-arusi Wake nguvu na mamlaka vitarudishwa kwetu! Kwa hiyo ili tuwe mfupa wa mfupa Wake lazima tufungwe pamoja kwa nguvu. Ili kuwa dutu na nguvu ya mwili, lazima pia tuwe mfupa wa mfupa Wake unaotufanya wamoja Naye, mwili sawa na Kristo!
Unapotafuta neno Bibi arusi katika Strongs Concordance ina maana ya kukamilisha, kufanya ukamilifu. Kwa hiyo tena, ili tuwe wakamilifu lazima tuwe mfupa wa mfupa Wake!
Nilipokuwa nikitafuta mambo kwenye kamusi ya Strongs, nilijitenga na kutafuta neno kushinda. Sasa naweza kuona kwa nini Mungu anataka watu wake wakusanyike siku ya Sabato na Sikukuu! Neno kushinda maana yake, jikusanye, jikusanye pamoja katika majeshi. Askari maana yake ni askari, wapiganaji, hmm, unaweza kuona Bibi-arusi ni msaada muhimu sana kwa mwili wa Kristo! Kwa kuwa yeye ni mfupa wa mfupa Wake, ana nguvu na nguvu zinazohitajika ili kuwa mshindi. Amejizatiti kwa ukweli ili asiwe shabaha rahisi kwa Babeli kupotosha kupitia uwongo wake na mafundisho yaliyopotoka pia. Adui anapozungusha upanga wake wa maarifa yaliyopotoka, yeye atumia upanga wa kweli, akilazimisha ushindi wa Yeshua juu ya ulimwengu wa Shetani, kazi zake na majeshi yake kama inavyoonekana kwenye Waefeso 6.
Mwishoni, hizi ni nyakati zenye kusisimua na tunakaribia kuona Isaya 11 ikitimizwa. Kweli inabebwa duniani kote kwa upepo na wale wanaomtafuta Mungu na Ufalme Wake wanaisikia katika roho zao na wanakua na kufanana na Baba yao. Kwa kila ukweli mpya haya yanakaribia kuwa katika upatano, katika kusawazisha na mapenzi ya Mungu na viumbe vingine vyote vitafuata mfano huo. Sio wazao wa Adamu tena, tumezaliwa kupitia Yeshua, elohim, watoto wa Mungu.
Bofya vichwa ili kucheza nyimbo zinazohusiana na mada hii
Children Of The Light
A New And Different Kind
We Are Elohim

Tumia (+) kupanua uorodheshaji ndani ya kikundi.

2020 + -
2015 + -
2012 + -
2011 + -

Submit Your Site To The Web's Top 50 Search Engines for Free!